Mtaalamu wa Chai kutoka Bodi atembelea shamba la chai 
                        
                    
                
            
                            Mtaalamu wa Chai kutoka Bodi atembelea shamba la chai 
                        
                    
                        
                             Imewekwa: 19 Jan, 2025
                        
                    
                
                    Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Machare Estate, Madam Bente ( katikati) akiwa na Meneja wake(kushoto) pamoja na Mtaalamu kutoka Bodi ya Chai Tanzania (TBT) wakati Mtaalamu huyo alipotembelea shamba la Machare.
Kampuni hiyo ya Machare Estate inamiliki kiwanda cha kuchakata majani mabichi ya chai kwa ajili ya kupata chai kavu maalumu yaani orthodox tea.
Akiwa katika kiwanda hicho alipata wasaha wa kutembelea Maabara ya Chai iambapo ndani yake ndipo chai inaandaliwa kwa ajili ya uonjaji baada ya kutengenezwa.
Pia alipata wasaha wa kuona chai mbalimbali zikiwemo ambazo hazijafanyiwa uchachuaji yaani "unfermented tea" pamoja na zile ambazo zimefanyiwa uchachuaji " fermented teas'".